Kwanza tunasikia jinsi alivyoitwa na Mungu juu ya mlima pale Kenya. Halafu tunasoma moja ya mahubiri ya Isaya. Na baadaye tunamfuata katika njia yake ndefu ya kupata ubatizo. Halafu tutaangalia huduma yake: Mhubiri Isaya na ujumbe
wake, mpatanishi na mbinu zake, marafiki zake Joshua na Isaaka. Tutaangalia kazi yake katika Tanzania na tutasikiliza wenye hoja zao Kenya wasemavyo. Pia tutajaribu kujibu maswali: Je, Isaya Ole Ntokoti ni Oloiboni bado? Au ni mtu mwenye wito maalum wa Mungu kama nabii?